UJASIRIAMALI KAMA KAZI


ujasiriamali kama kazi

Nimesha eleza sana juu ya dhana ya ujasiliamali katika blog(gjobu.blogsport.com) hii hivyo si vizuri nikirudia. Ujasiliamali kama kazi hapa nalenga kuonyesha ni jinsi gani mtu anaweza kujiajiri kama mjasiliamali na kuachana na mawazo ya kuajiriwa. Kuwa na mtaji peke haitoshi ili mtu aweze kujiajiri bali mjasiliamali anahitaji kujua na kuvifanyia kazi vitu vifuatavyo ambavyo ni jinsi ya kupata wazo la biashara,kugundua na kutambua biashara sahihi,vigezo muhimu wakati wa kuchagua biahara ya kufanya,vitu muhimu vya kufuata wakati wa kuanzisha biashara na kazi za mjasiliamali.
Kabla hujanzisha biashara jiulize maswali yafuatayo
  •       Kwanini unataka kuanzisha biashara?
  •       Je upo tayari kufanya biashara?
  •       Je unamalengo gani katika biashara hiyo?
  •       Je unaujuzi na elimu ya  kutosha katika kunzisha,kuendesha    na kukua kibiashara?
  •       Mtaji kiasi gani unahitajika ili kuanzisha biashara?
  •       Biashara ya pekeyako au ya ushirikiano?

Jinsi ya kupata wazo la biashara

  •   Tafuta msaada toka kwa wote ambao wapo katika biashara,watakwambia vitu muhimu katika biashara.
  •   Angalia wengine wanafanya nini, tambua matatizo wanayokumbana nayo na kisha fikiri njia sahihi za kutatua matatizo hayo.
  •  Jadiri pamoja na marafiki na jamaa wa karibu juu ya kile unchotaka kufanya
  •  Kuwa mdadisi kwa kuchunguza vitu kwa makini,tembelea maeneo mengine ili kujua wanafanya nini
  •   Fikiri kufanya kiu kipya ambacho hakijafanywa katika eneo ulilopo

Faida za kuwa na wazo la biashara

  1.  Hupunguza vikwaazo katika kuendesha biashara
  2.     Husaidia katika kufanya maamuzi sahihi ya biashara gani uanzishe\
  3.    Kupata mafanikia katika biashara
  4.     Ni hamasa kubwa katika kuingia katika biashara

Jinsi kuugundua na kutambua biashara sahihi

  •  Kuwa makini katika kuchaga aina ya biashara ya kufanya
  • chagua kulingana na uwezo wako katika kuendesha biashara hiyo
  •  chagua biashara unayo ipenda kwani uwezekano wa kuifanya vizuri ni mkubwa
  • amua biashara ya kufanya hasa bada ya kufanya uchunguzi wa kutosha na kutafuta habari za kina juu ya biashara husika hi itakusaidia kufanya biashara bilia vikwazo vingi

vigezo muhimu wakati wa kuchagua biashara ya kufanya

v  uwezekao a kufanikiwa
v  kupata faida
v  kutambua vikwazo katika bishara
v  biashara inayo vutia
v  elimu ya biashara pamoja na rasilimali watu
v  mtaji
v  masoko
v  upatikanaji wa stoo za kuhifadhia bidhaa
v  upatikanaji wa malighafi
v  usafiri
v  uwezekano wa kupata msaada toka serikalini

kazi ya mjasiliamali

  1.      kuaandaa mpango wa biashara
  2.       kuatafuta mtaji
  3.      kupanga bei
  4.       kutunza kumbukumbu za biashara
  5.      kutunza fedha
  6.       kujitegemea
  7.     kuchanganua gharama
  8.      kutangaz bidhaa anazouza
  9.      kubaini vikwazo katika biashara
  10.     ubunifu




 Ufunguo wa mafanikio katika ujasiliamali

mpango  biashara

kabla hujaanza biashara hakikisha unaandaa/kuandika mpango biashara madhubuti ambao utaeleza kipi utafanya na mpangilio mzima wa biashara yako. Pia fikiri kuhusu kesho, wiki ijayo na tazama mbele zaidi

dondo

  •  tambua mambo yanaenda yakibadirika hivyo nawe badirika kulinga ana wakati pomoja na mazingira
  •  tambua kuwa huwezi fanya kila kitu pekeyako
  •   mjasiliamali mzuri ni yule anaye  fikiri na kutazama mbele (future oriented)
  •   mjasiria mali mzuri ni yule anayetumia muda vizuri
  •   mpango biashara utakusidia kuona fulsa mpya na chagamoto mbalimbali katika biashara zako
  •   tafuta ushauri toka kwa wataalamu mbalimbali wa biashara na ujasiliamali kwa kile unacho kifanya
  •   uthubutu ni ufunguo wa mafanikio katika ujasiliamali.

Jinsi ya kupata mafanikio katika biashara

Kunanjia nyigi unaweza kuzitumia ili kufikia mafanikio katiaka biashara baadhi ni kama zifuatazo.
Fikiri kuhusu……

  1.     jinsi ya kubadiri wazo la biashara na kuwa biashara
  2.      imarisha na ongeza ubora wa bidhaa na huduma unazotoa
  3.     gundua,tambua na anzisha bidhaa mpya na huduma
  4.      vutia wateja
  5.      simamia biashara yako hata kama haupo (weka wasaidizi)
  6.      ongeza juhudi
  7.     ajiri wasaidizi bora


jitofautishe katika utoaji wa huduma na bidhaa

kwanini wateja waje kwako?

Kujitofautisha katika kuuza bidhaa na aina ya huduma unayotoa ni kitu muhimu hii itasababisha wateja weni wafuate huduma zako,wafanya biashara wengi wanaamini kuwa kupunguza bei ni kivutio kikubwa cha wateja katika biashara, lakini sio bei tu ianayo weza kuvutia wateja wengi katika huduma zako, wateja wengi huthamini huduma bora na bidhaa bora kama ifuatavyo….
  •    Ubora wa bidhaa yenyewe nahduma unazo toa
  •         Urahisi wakupata huduma na bidhaa zako
  •         Upatikanaji wa bidhaa na huduma (je zina patikana muda wote?)
  •         Usalama wa bidhaa na huduma zako
  •        Je bidhaa au huduma zako haziharibu mazingira
  •         Bidhaa zako zimezalishwa wapi?......nchini au ughaibuni.
  •         Maoni  ya wateja wako juu ya bidhaa na huduma unazotoa, wanasemje juu ya bidhaa na huduma zako
  •          Kilasiku buni na fikiri njia mbali mbali ambazo zitafanya wateja apende bidhaa zako zaidi.


4 comments:

  1. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  2. je unataka kusoma,kutimiza malego
    kama kujenga nyumba kununua gari au unatafuta
    ajira na ungependa kupata msaada.

    tunatoa usaidizi katika yote haya. bila hati ya nyumba au ya gari utaweza kupata mkopo usiokuwa na riba.karibu sana
    BONYEZA link http://4ui.us/pataunachotaka Kwa taarifa za kina.

    ReplyDelete
    Replies
    1. This comment has been removed by the author.

      Delete